DEO MECK Apongeza CCM kwa Kumchagua Stephen Wasira Kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Bara
Pichani ni Mdau wa Maendeleo na kada wa Ccm Ndg DEO MECK Mwanachama na mdau wa maendeleo, Deo Meck, amepongeza Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa kumchagua Stephen Wasira kuwa Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara. Meck amesema kuwa uteuzi huo ni hatua sahihi kwa chama, kwani Wasira ni kiongozi mwenye uzoefu mkubwa, anayejua misingi ya chama, na mwenye maono thabiti kwa maendeleo ya taifa. Akizungumza na waandishi wa habari, Meck alisema kuwa Wasira ana rekodi nzuri ya uongozi, akibainisha kuwa amekuwa mstari wa mbele katika kuhimiza nidhamu, umoja, na mshikamano ndani ya chama. Alisisitiza kuwa uamuzi wa CCM kumchagua Wasira unaonyesha kuwa chama kinatambua mchango wa viongozi wenye uadilifu na walio tayari kuendeleza misingi ya chama kwa manufaa ya Watanzania wote. "Wasira ni mtu makini, ana uzoefu wa muda mrefu ndani ya chama na serikali. Amejitoa kwa hali na mali kuhakikisha kuwa misingi ya chama inaheshimiwa na maendeleo ya wananchi yanapewa kipaumbele. Uteuzi wake ni wa busara, ...