Posts

MBUNGE ESTHER BULAYA ASHIRIKI HAFLA YA UGAWAJI WA SARUJI MKOA WA MARA

Image
Pichani ni Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini akipokea Saruji Toka Nyansaho foundation Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Esther Bulaya, tarehe 22 Machi 2026 alishiriki katika hafla ya ugawaji wa mifuko ya saruji iliyofanyika katika ukumbi wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Mara uliopo Musoma. Hafla hiyo ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kisiasa kutoka majimbo ya Mkoa wa Mara pamoja na wananchi waliokusanyika kushuhudia tukio hilo muhimu la maendeleo. Hafla hiyo iliandaliwa na Nyansaho Foundation chini ya uongozi wa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa, Rhimo Nyansaho, ambaye pia alikuwa mgeni rasmi katika tukio hilo. Taasisi hiyo imekuwa ikifanya shughuli mbalimbali za kijamii zenye lengo la kusaidia jamii katika maeneo tofauti ya maendeleo. Lengo kuu la hafla hiyo lilikuwa ni kugawa mifuko ya saruji kwa majimbo yote 11 ya Mkoa wa Mara. Msaada huo umetolewa kwa lengo la kusaidia utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika jamii, ikiwemo ujenzi wa miundombinu muhimu kama shule...

BULAYA AUNGANA NA VIJANA BODA BODA, ATOA MSAADA NA KUHIMIZA AMANI

Image
                            PICHANI NI  MHE. ESTHER BULAYA AKIWA NA MAAFISA USAFILISHAJI WA BUNDA STOO Na mwandishi wetu Bunda mjini  Mbunge wa Jimbo la Bunda Mjini, Esther Bulaya, ametembelea vijana wa kituo cha bodaboda Bunda Stoo na kushiriki nao mazungumzo yenye kujenga mshikamano na maendeleo ya vijana. Katika ziara hiyo, Mhe. Bulaya alionyesha kuguswa na hali ya kijiwe chao na kutoa msaada wa kiasi cha shilingi 250,000 kwa ajili ya ukarabati, ili kuboresha mazingira yao na kupata kivuli bora wakati wa shughuli zao za kila siku. Bulaya akiteta na maafisa usafilishaji Aidha, alimsaidia kijana mmoja kwa kumpatia fedha za kufanya marekebisho ya pikipiki yake, akilenga kuongeza usalama barabarani na kuboresha kipato chake kupitia kazi ya usafirishaji. Mbali na misaada hiyo, Mhe. Bulaya alitoa elimu na mawaidha kwa vijana hao, akiwataka kuwa makini na watu wanaoweza kuwatumia vibaya kwa maslahi binafsi. Aliw...

Kisangwa Yapata Neema ya Maji: Esther Bulaya Ashiriki Uzinduzi wa Mradi wa Milioni 716 Bunda

Image
MBUNGE WA BUNDA MJINI MHE. ESTHER BULAYA    Wananchi wa Kata ya Mchalo, tawi la Kisangwa, Wilaya ya Bunda wamepata tumaini jipya baada ya kuzinduliwa rasmi kwa jiwe la msingi la mradi wa maji unaolenga kuondoa changamoto ya uhaba wa huduma hiyo muhimu. Mbunge wa Bunda Mjini, Esther Bulaya, leo Machi 17, 2026 alishiriki katika uzinduzi huo uliokwenda sambamba na maadhimisho ya Wiki ya Maji, tukio lililokusanya viongozi wa kisiasa, wataalamu wa sekta ya maji pamoja na wananc hi wa eneo hilo. Uzinduzi huo uliongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Aswege Enock Kaminyoge, aliyemwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Mara, Evans Mtambi, huku ukihudhuriwa pia na Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Bunda (BUWASA), Esther Enock Gilyoma, pamoja na viongozi mbalimbali wa idara ya maji. Akizungumza katika hafla hiyo, Bulaya alieleza kuwa mradi huo wenye thamani ya shilingi milioni 716 ni sehemu ya jitihada za Serikali kuhakikisha wananchi wanapata huduma safi na salama ya maji, huku ...

Mheshimiwa Esther N. Matiko Aanza Ziara Tarime Mjini kwa Kishindo, Aahidi Kutatua Kero za Wananchi

Image
 Mbunge wa Tarime Mjini, Esther N. Matiko, ameanza rasmi ziara yake jimboni kwa kishindo kwa kutembelea Kata ya Ketare, ambapo amekutana na wananchi, kusikiliza changamoto zao na kuahidi kuzifanyia kazi kwa haraka. Asikiliza Kero za Wananchi Ketare Katika mkutano uliofanyika Ketare, wananchi walipata nafasi ya kuwasilisha kero mbalimbali zinazowakabili, ikiwemo changamoto za miundombinu ya barabara, huduma za maji, na masuala ya maendeleo ya kijamii. Mbunge huyo alisisitiza kuwa lengo la ziara yake ni kusikiliza sauti za wananchi moja kwa moja ili kupata uhalisia wa changamoto zilizopo na kuzitafutia ufumbuzi wa kudumu. Alieleza kuwa ofisi yake itaendelea kushirikiana na viongozi wa serikali za mitaa na mamlaka husika kuhakikisha kila hoja inayowasilishwa inapewa uzito unaostahili. Serikali Yatenga Fedha kwajili ya Nyamwaga Road Akizungumzia kwa kina kero ya barabara ya Nyamwaga Road, Mbunge huyo alisema kuwa tayari Serikali imetenga kiasi cha fedha kwa ajili ya ujenzi na uboreshaj...

MKURUGENZI WA SOYA ONE LIMITED AWASISITIZA WAUMINI WA EAGT RONSOTI TARIME MJINI KUILINDA AMANI; AFANIKISHA UPATIKANAJI WA MCHANGO WA MILIONI 12, ACHANGIA MILIONI 8 NA ASINDIKIZWA KWA MILIONI 5

Image
MKURUGENZI WA SOYA ONE LIMITED  (CHACHA GESORA)  Tarime Mjini, Tanzania – Mkurugenzi wa Soya One Limited, Chacha Soya, ameendelea kuonyesha moyo wa kujitoa kwa jamii baada ya kufanikisha upatikanaji wa mchango wa jumla ya shilingi milioni 12, ambapo mwenyewe alichangia milioni 8, na waumini pamoja na wageni wengine wakasindikiza kwa milioni 5. Mkurugenzi huyo alialikwa rasmi kama mgeni maalum katika ibada ya Jumapili iliyofanyika katika Kanisa la EAGT Ronsoti, ibada iliyojaa uwepo wa Mungu na iliyoongozwa na Mchungaji Maswi. Katika hotuba yake yenye kugusa mioyo, Mkurugenzi Soya alisisitiza umuhimu wa kulinda amani ya nchi akisema: “Amani yetu ni nguzo ya maendeleo. Tanzania imebarikiwa na Mungu kwa utulivu wake. Tuilinde, tuiombee, na tuishi kama watu wanaothamini urithi huu adhimu.” Alisisitiza kuwa amani ndiyo msingi wa ibada, biashara, uchumi na ustawi wa familia, hivyo kila Mwanatarime na Mtanzania kwa ujumla ana wajibu wa kuwa mlinzi wa amani. Katika kuendelea kusapoti k...

KWA NINI SAMIA SULUHU HASSAN ANASTAHILI KURA ZA USHINDI KWA MARA NYINGINE

Image
DR SAMIA SULUHU HASSAN Na Daniel Mussa MBC MEDIA Tanzania iko katika kipindi cha mageuzi makubwa ya maendeleo, umoja, na diplomasia chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan. Tangu aingie madarakani mwaka 2021, Mama Samia amethibitisha kwa vitendo kuwa ni kiongozi mwenye maono, busara, na moyo wa kujenga taifa linaloangalia mbele. Ni kutokana na kazi yake kubwa na dira yake thabiti, Watanzania wana kila sababu ya kumpa tena kura za ushindi ili aendelee kuiongoza nchi kwa kipindi kingine cha miaka mitano. Kwanza, Mama Samia amerejesha heshima ya Tanzania kimataifa. Kupitia diplomasia yake ya ucheshi, usikivu na utulivu, ameweka taifa katika ramani ya dunia. Leo hii Tanzania ni kivutio kwa wawekezaji, watalii, na mashirika ya kimataifa, jambo lililoongeza ajira na kipato cha taifa. Pili, ameweka msukumo mkubwa katika maendeleo ya watu. Kupitia miradi mikubwa ya elimu, afya, maji na miundombinu, Mama Samia amegusa maisha ya Watanzania moja kwa moja. Elimu bure imepanuliwa, huduma za af...

ALKOS ELUTION PLANT YAIKONGA SOYA ONE LIMITED KWA USHIRIKIANO MZURI NA JAMII

Image
PICHANI NI WAFANYAKAZI WA SOYA ONE LIMITED PAMOJA NA ALKOS ELUTION WAKIWA NA VIONGOZI WAO Na Daniel Mussa, MBC Media Online News – Tarime TARIME, Oktoba 2025 Kampuni ya Alkos Elution Plant, inayojihusisha na uchenjuaji wa madini na yenye makao yake mtaa wa Zaka Filling, Nkende  Tarime Mjini, imeipongeza kampuni ya Soya One Limited kwa kuwa mdau mkubwa wa maendeleo na mshirika wa kweli wa jamii. Akizungumza katika hafla ya kuadhimisha Wiki ya Mteja iliyofanyika katika ofisi za Alkos Elution Plant, viongozi wa kampuni hiyo walimshukuru Mkurugenzi wa Soya One Limited, Ndugu Chacha Soya, kwa kukubali mwaliko wao na kuhudhuria kama mgeni rasmi katika tukio hilo muhimu. Kwa mujibu wa viongozi wa Alkos Elution Plant, ushirikiano kati ya kampuni hizo mbili umechangia kuimarisha uhusiano kati ya sekta binafsi na jamii, sambamba na kusaidia utekelezaji wa miradi ya kijamii na maendeleo ya kiuchumi ndani ya Wilaya ya Tarime. “Tunampongeza Ndugu Chacha Soya kwa moyo wake wa uzalendo na ushirik...