SOYA ONE LIMITED YAMUUNGA MKONO MHANDISI WA MADINI MKOA WA MARA, YAMPA PONGEZI KWA UTENDAJI WAKE BORA
PICHANI NI MHANDISI MSUYA OFISI YA MADINI MKOA WA MARA Tarime, Juni 7, 2025 Kampuni ya Soya One Limited chini ya uongozi wa Mkurugenzi wake mahiri, Chacha Soya, imetoa pongezi za dhati kwa Mhandisi wa Madini Mkoa wa Mara, Mhandisi Amin Msuya, kwa kazi nzuri na ya mfano anayofanya katika kusimamia sekta ya madini mkoani humo. Kupitia taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa leo, Chacha Soya alisema kuwa kampuni yake, ambayo inajihusisha na shughuli za uchimbaji na usimamizi wa madini kwa kuzingatia misingi ya uwajibikaji kwa jamii, imeridhishwa na namna ambavyo ofisi ya Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mara inatekeleza majukumu yake kwa weledi, uwazi na kasi inayolenga maendeleo ya wachimbaji na ustawi wa uchumi wa mkoa. > "Kwa niaba ya Soya One Limited, napenda kumpongeza Mhandisi Amin Msuya kwa kazi nzuri anayoifanya. Ameonesha mfano wa uongozi bora kwa kushirikiana na wadau wote wa sekta ya madini bila ubaguzi, huku akihakikisha mazingira rafiki ya uwekezaji na uchimbaji yanaim...