Posts

Showing posts from October, 2024

HAYA HAPA KWENYE MAGAZETI YA LEO ALHAMISI OKTOBA 31, 2024

Image
Home Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania October 31, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za nyuma za Magazeti ya Tanzania magazetini Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia moonglobal255@gmail.com au WhatsaApp:  +255656114499

ANGALIA MATOKEO YA DARASA LA SABA HAPA

Image
  NATIONAL EXAMINATIONS COUNCIL OF TANZANIA PSLE-2024 EXAMINATION RESULTS ARUSHA DAR ES SALAAM DODOMA IRINGA KAGERA KIGOMA KILIMANJARO LINDI MARA MBEYA MOROGORO MTWARA MWANZA PWANI RUKWA RUVUMA SHINYANGA SINGIDA TABORA TANGA MANYARA GEITA KATAVI NJOMBE SIMIYU SONGWE

MATOKEO ya Mtihani wa Taifa wa Darasa la Saba Mwaka 2024 yamedhihirisha ubora wa Shule ya Royal Family School

Image
  MATOKEO ya Mtihani wa Taifa wa Darasa la Saba Mwaka 2024 yamedhihirisha ubora wa Shule ya  Royal Family School (pichani juu),iliyopo Geita Mjini Shule hiyo ambayo inajulikana kwa jina la  Royal Family School iling’ara katika matokeo hayo, chini ya uongozi wa Royal Family School Royal Family School ambayo ni shule ya kutwa na bweni, ilipata ufaulu wa juu  Sana WAZAZI na walezi leteni watoto wenu wapate elimu bora katika mazingira ya kuvutia na wezeshi ya kujifunza kwa weledi hapa Royal Family School.” “Hakuna mzazi aliyejutia kumleta mtoto wake kusoma katika shule hii. Tuna kila sababu ya kuwathibitishia Watanzania kuwa shule yetu ni mkombozi wa elimu bora,” anasema. Royol Family School, ni shule ya kisasa ya bweni na kutwa kwa wanafunzi Ni mradi mkubwa wa kijamii uliofanikishwa na mwekezaji mzawa

OROMBE CUP YAMALIZIKA SUSUNI ,WAISHUKURU SOYA ONE LIMITED KWA KUWA CHACHU YA MAENDELEO KWENYE JAMII

Image
  Na Ernest Makanya  mashindano ya Orombe Cup yaliyokuwa yakifanyika katika uwanja wa Shule ya msingi Susuni  mashindano hayo yamemalizika Jana Agositi 28,2022 ambapo mshindi wa kwanza alipata zawadi ya shilingi  Laki tatu huku mshindi wa pili. alipata laki mbili  Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi hizo Afisa Tarafa Ndg Gradnes mtandu kwa Niaba ya Mkuu wa Wilaya Ya tarime Meja Edward Gowere amepongeza Wananchi Kujitokeza kwa wingi kwenye Fainal za michuano hiyo alisema mashindano hayo yamekuwa chachu katika Tarafa Ya Ichungu kwa kuhamasisha vijana kuto Jihusisha na mambo yanaweza kuharibu amani  Gradnes ametoa wito kwa wakazi wa Wilaya Tarime kuwa wazalendo Pia Kujitokeza kwa Wingi Kushiriki Uchaguzi wa Serikali za Mitaa. Akizungumzia Mafanikio ya Michuano hiyo Diwani Viti MaalumTarafayaIchungu Mhe Josephine  Orombe,amesema kuwa Alishawishika zaidi Kuwekeza kwenye michezo kwani michezo inawaleta watu pamoja hata hivyo Mhe Orombe Ameishukuru Soya...

HAYA HAPA MAGAZETI YA LEO JUMANNE OKTOBA 29, 2024

Image
Good Morning Mtu wangu wa nguvu kutoka Tanzania October 29, 2024,nakukaribisha kutazama kile kilichoandikwa katika kurasa za mbele na za nyuma za Magazeti ya Tanzania Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia moonglobal255@gmail.com au WhatsaApp: +255656114499

CHONCHORIO ALIVYO ONGEZA MVUTO ZOEZI LA UCHUKUAJI WA FOMU ZA KUGOMBEA SERIKALI ZA MITAA JIMBO LA TARIME MJINI

Image
Na Ernest makanya, Tarime Mjini   Maandamano yaliyo anzia Ofisi Za Chama Cha Mapinduzi Wilaya Ya Tarime Kuelekea Kwenye Vituo Vya kuchukuria Fomu Za Kugombea Serikali Za Mitaa Yameongozwa na Mjumbe Wa Mkutano Mkuu Wa Ccm Taifa Ndg Daniel Chonchorio ambapo wagombea nafasi za uenyeviti wa mitaa Jimbo la Tarime Mjini wakienda kuchukua fomu ofisi ya msimamizi wa uchaguzi wa serikali  Baadhi ya wagombea nafasi ya uenyeviti wa mitaa kupitia Chama cha Mapinduzi CCM Wameongozana na Mjumbe wa Mkutano Mkuu Wa Ccm Taifa Ndg Daniel Chonchorio Wamepita kila kituo Kuhakikisha zoezi Linakwenda vizuri Wagombea saba  nafasi ya Mwenyekiti wa serikali za mitaa kupitia Ccm Wilaya Ya Tarime wamechukua fomu za serikali za kugombea nafasi hiyo katika uchaguzi ujao wa serikali za mitaa Novemba 27 mwaka huu. Zoezi hilo limefanyika Leo Oktoba 28,2024 likiambatana na maandamano ya kutembea kwa miguu kuanzia Ofisi Za Chama Cha Mapinduzi Wilaya Ya tarime kuelekea ofisi ya msimamizi wa uchaguz...

WAZIRI CHANA AELEKEZA ASKARI UHIFADHI KUWEKA KAMBI IKUNGI KUKABILIANA NA TEMBO

Image
  Na Happiness Shayo -Ikungi Waziri wa Maliasili na Utalii,Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) ameelekeza timu ya Askari Uhifadhi 18 kuweka kambi katika Halmashauri ya Wilaya ya Ikungi Mkoani Singida kwa lengo la kukabiliana na tembo wanaovambia makazi ya watu. Hatua hiyo inafuatiwa na tukio la hivi karibuni la tembo kuwepo katika eneo hilo na kusababisha taharuki kwa wananchi. Akizungumza na wananchi katika Mkutano wa hadhara leo Oktoba 28,2024 kwenye Kijiji cha Mkiwa Wilaya ya Ikungi, Mkoani Singida Mhe. Chana amesema nia ya Serikali ni kuhakikisha changamoto ya wanyamapori wakali na waharibifu hususan tembo inapungua au kumalizika kabisa. "Tunakwenda kuongeza askari watakaotusaidia kuhakikisha tembo wanarudi katika maeneo yao ya hifadhi sambamba na kuongeza mabomu baridi kufukuza tembo" Mhe. Chana amesisitiza. Aidha, amesema Wizara ya Maliasili na Utalii kwa kushirikiana na Serikali za Vijiji,Wilaya na Mkoa itafanya zoezi la kutambua na kuweka alama katika maeneo ya Korido...

WAZIRI CHANA AHAMASISHA WAWEKEZAJI WA MAZAO YA MISITU KUANZISHA VIWANDA NCHINI

Image
  Na Happiness Shayo - Mafinga Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) amewahimiza wawekezaji wa mazao ya misitu kutoka nchini China kuanzisha viwanda kwa lengo la kuuza bidhaa zilizokamilika kwa ajili ya masoko ya nje ya nchi. Ameyasema hayo leo Oktoba 27,2024 wakati wa uzinduzi wa Umoja wa Wawekezaji wa Mazao ya Misitu wa China nchini Tanzania uliofanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Mji wa Mafinga Mkoani Iringa. "Nawapongeza mnaozalisha bidhaa zilizokamilika ambao tayari mna viwanda lakini tuendelee kuwekeza kwa kufuata taratibu na sheria" amesema Mhe. Chana huku akisisitiza "Tunataka Tanzania ya Viwanda". Amefafanua kuwa kupitia umoja huo mashirikiano na mahusiano kati ya Serikali na wenye viwanda yatakuwa rahisi zaidi na kusisitiza kuwa bidhaa zitakazozalishwa ziwe na nembo ya "made in Tanzania". Naye, Rais wa Umoja wa Wawekezaji wa Mazao ya Misitu wa China nchini Tanzania, Bw.Zheng RONGNAN amesema kwa kushirikiana na Ser...

VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI OKTOBA 27, 2024 DK.MWINYI NITAWAJIBU KWA VITENDO

Image
  VICHWA VYA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI OKTOBA 27, 2024 DK.MWINYI NITAWAJIBU KWA VITENDO