SAID CHAMBIRI AWEKA WAZI SAFARI YAKE YA SIASA ,AWAOMBA WANANCHI KUKIWAAMINI VIONGOZI WA CCM NA KUKIPA CHAMA( CCM) USHINDI
Na Mwandishi Wetu
Kada wa chama cha Mapinduzi CCM na Mdau wa Maendeleo Said Chambiri Ambaye Pia Ni Mkurugenzi wa Hotel ya HillsideHotel iliyopo Tarime Ameieleza MBC MEDIA Juu Ya Safari yake ya Siasa Ndani ya Chama Cha Mapinduzi
Said Chambiri Ameeleza Pia Sababu Za yeye Kuwa karibu na Chama Cha Mapinduzi
Mimi nimezaliwa hapa hapa tarime na nimesoma hapa tarime Elimu Yangu Ya Juu nimepata Inje ya Tarime Lakini Pia
Nimewekeza Tarime ninayo hotel ya kisasa inaitwa HillsideHotel @hillside_hotel_and_safaritours Mimi Mimi
Nimefanya siasa inje ya Tarime Nipata Bahati Ya kushiriki kwenye program za Chama Nyingi Ndani ya Tarime Na Inje ya Tarime
Nimefanya kampeni Jimbo la babati mjini na kufanikiwa kurudishwa ndani ya ccm
Pia nimefanya kampeni temeke
Na katika uchaguzi pia nimeshiriki Chaguzi Nyingi Sana Pia ikumbukwe kuwa
Mimi ni mwanachama wa ccm Kwa muda Mrefu nimejiunga kwenye jumuiya ya uvccm mwaka 2004
Nimeshawishika kuendelea na shughuri za siasa kwenye mji wa tarime kwa sababu ndo sehemu ambayo naishi na
Sasa tunaende kwenye ushindani wa Vyama pinzani hivyo Sisi kwa Wanachama Tunapaswa kukipa Chama Chetu Nguvu
Lakini Pia Mimi Niweke wazi kuwa kwa sasa mimi sio mtia nia Ndani Ya Chama Chetu Ni wajibu Wetu kama wanachama sehemu yoyote unayo kuwa unaruhusiwa kuendelea na Shughuri za kichama Kwa Sasa nipo Tarime Hivyo Kama Mwanachama ninatakiwa kushiriki kwenye Shughuri Za Kichama Kuhakikisha Chama Chetu Kinapata Ushindi wa Kishindo
Mimi ninapo kuwa sehemu ninafanya kazi ya Chama kama Mwanachama Pia ikumbukwe kuwa mimi nimewekeza tarime sheria inanitaka kurudisha asilimia kadhaa kwenye jamii
Mfano mimi ninapo alikwa sehemu kama mgeni natoa pale kama mdau Kingine watanzania wanapaswa kukijua ni kwamba
Mimi ninapata faida nyingi na Serikali ya mama samia
Kama Mwanachama wa Ccm Ninapaswa kuwa karibu na Jamii yangu ili kusaidia Shughuri Za Maendeleo na Kumsapoti Mhe mbunge wetu Michael Kembaki Kwa sababu
Hatuwezi Kumuachia majukumu yote yeye kutoa msada kumsubiria mbunge afanye mambo yote Tunaweza kujikuta tunapoteza hivyo sisi kama wanachama inabidi tufanye mambo mengine kutimiza adhima ya chama chetu na tukisema tunamuachia mbunge kazi zote hato weza tunaweza kwenda kupoteza na kinapopoteza chama hajapoteza mbunge kimepoteza chama
Tupo kwenye safari ya kukiimarisha chama chetu "Amesema Said Chambiri"
Pia Saidi Chambiri Amewataka Wanachama na Wananchi Kujitokeza kwa wingi kushiriki kwenye Uchaguzi Wa Serikali za Mitaa Na kukiamini Chama cha Mapinduzi


Comments
Post a Comment