Posts

SOYA ONE LIMITED YAENDELEA KUNG’ARA KATIKA UDHAMINI WA ELIMU NA JAMII TARIME

Image
  Pichani Ni Mkurugenzi wa Soya One Limited ndg Chacha Soya akiwa na viongozi wa serikali Tarime, Mei 20, 2025 – Kampuni ya Soya One Limited inaendelea kudhihirisha dhamira yake ya dhati ya kusaidia jamii kupitia mchango wake mkubwa kwa shule na taasisi za kidini wilayani Tarime, ikiwa ni sehemu ya kaulimbiu yake ya “Jamii Kwanza.” Katika hatua hii kampuni hiyo imetoa gunia 10 za mahindi kwa shule za msingi Sabasaba, Mapinduzi na Azimio, kwa ajili ya chakula kwa wanafunzi. Pia, imeshughulikia gharama za kuunganishiwa umeme katika shule hizo tatu kwa kiasi cha Shilingi 836,577.52, hatua inayolenga kuboresha mazingira ya kujifunzia na kuongeza ufaulu. Kwa kuguswa na hali ya mwanafunzi mmoja mwenye changamoto ya kifedha, kampuni hiyo imetoa Shilingi 100,000 kumuwezesha kupata mahitaji muhimu ya shule na kuendelea na masomo bila vikwazo. Soya One Limited pia imeelekeza msaada wake kwa Shule ya Msingi Magufuli ya watoto wenye mahitaji maalum kwa kutoa gunia tano za mahindi, sukari na ho...

MANCHARE HECHE ATOA MCHANGO WA MILIONI MOJA NA MAJI KATONI 40 KATIKA KIKAO CHA HALMASHAURI KUU CCM TARIME

Image
PICHANI NI MJUMBE MKUTANO MKUU CCM TAIFA NDG MANCHARE HECHE Habari kamili Na Daniel Mussa Tarimee, Mei 19, 2025 Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, Wakili Manchare Heche, ameendelea kuonesha moyo wa kizalendo na kujitoa kwa ajili ya chama kwa kuchangia kiasi cha shilingi milioni moja pamoja na katoni 40 za maji katika kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Tarime kilichofanyika jana, Mei 18, 2025, mjini Tarime. Mchango huo umetolewa ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za chama katika kuimarisha shughuli zake za kisiasa na kiutendaji ndani ya Wilaya ya Tarime. Tukio hilo limepokelewa kwa furaha na pongezi kutoka kwa viongozi mbalimbali wa chama waliohudhuria kikao hicho, wakiongozwa na Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tarime. Akizungumza na MBC MEDIA mara baada ya kukabidhi msaada huo, Wakili Manchare Heche alisema kuwa anafanya hayo yote kwa lengo la kulisapoti Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili liendelee kuimarika na kuleta maendeleo kwa wananchi. Aidha, amepongeza...

Katibu Mkuu Eliakimu Chacha Maswi Achangia Milioni Moja Kufanikisha Mkutano wa Wajasiriamali Tarime

Image
  Pichani ni katibu mkuu wa katiba na sheria Eliakimu Chacha Maswi Tarime, Mei 16, 2025  Katika kuendelea kuunga mkono juhudi za kuwawezesha wanawake na vijana wajasiriamali nchini, Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Mheshimiwa Eliakimu Chacha Maswi, ameonesha mfano wa kuigwa kwa kuchangia shilingi milioni moja (1,000,000) kufanikisha mkutano wa mwezi wa wanawake na vijana wajasiriamali wa Wilaya ya Tarime. Mkutano huo muhimu umeandaliwa na Tanzania Women Chamber of Commerce (TWCC) kupitia ofisi yake ya Wilaya ya Tarime, na kufanyika katika ukumbi wa kisasa wa BlueSky, uliopo mjini Tarime. Tukio hilo limekusanya zaidi ya washiriki 150 kutoka kata mbalimbali za Wilaya ya Tarime, ambao ni wanawake na vijana wanaojihusisha na shughuli za ujasiriamali katika sekta tofauti kama vile kilimo, biashara ndogondogo, ushonaji, ufundi na utengenezaji wa bidhaa za mikono. Katika salamu rasmi zilizowasilishwa na mwakilishi wake, Katibu Mkuu Maswi alieleza kuwa mchango wake ni sehemu...

Mdau wa Maendeleo Musa Ryoba Achangia Maji Katika Mkutano wa Wanawake na Vijana Wajasiriamali Tarime

Image
Pichani ni Mkurugenzi wa mwanzo Mpya Ndg Musa Ryoba Tarime, Mei 16, 2025 Mdau wa maendeleo na Mkurugenzi wa Mwanzo Mpya Foundation, Musa Ryoba, ameonesha moyo wa uzalendo na kujitoa kwa jamii kwa kuchangia katoni 20 za maji kwa ajili ya kufanikisha mkutano wa mwezi wa wanawake na vijana wajasiriamali wa Wilaya ya Tarime. Mkutano huo muhimu umeandaliwa na taasisi ya Tanzania Women Chamber of Commerce (TWCC) na kufanyika leo katika ukumbi wa BlueSky, ukiwaleta pamoja wanawake na vijana walioko kwenye sekta mbalimbali za ujasiriamali kwa lengo la kujifunza, kubadilishana uzoefu na kujengewa uwezo wa kukuza biashara zao. Katika mchango wake, Musa Ryoba alisisitiza umuhimu wa kuwainua wanawake na vijana kupitia fursa za kiuchumi na elimu ya ujasiriamali. “Nimeguswa na jitihada za TWCC katika kuwawezesha wanawake na vijana, ndiyo maana niliona ni vyema kuunga mkono mkutano huu. Maji ni kitu kidogo lakini muhimu sana katika mazingira ya mkutano,” alisema. Mratibu wa mkutano huo kutoka TWCC al...

Matiko Foundation Yachangia Shilingi Laki Tano Katika Mkutano wa Wanawake na Vijana Wajasiriamali Tarime

Image
PICHANI NI KATIBU WA MATIKO FOUNDATION PETER MAGWI Tarime, Mei 16, 2025 – Taasisi ya kijamii ya Matiko Foundation imeendelea kudhihirisha dhamira yake ya kusaidia maendeleo ya jamii kwa kuchangia shilingi 500,000 kufanikisha mkutano wa wanawake na vijana wajasiriamali Wilaya ya Tarime, uliofanyika leo chini ya uratibu wa Tanzania Women Chamber of Commerce (TWCC). Mchango huo umetolewa rasmi na Katibu wa Matiko Foundation, Ndg. Peter Magwi, kwa niaba ya taasisi hiyo, ambapo aliipongeza TWCC kwa kuwaunganisha wanawake na vijana katika harakati za kujitegemea kiuchumi. Ndg. Peter Magwi alisema: "Matiko Foundation inatambua umuhimu wa kuwainua wanawake na vijana katika kila hatua ya maendeleo. Tunaamini kuwa kingamano ili ni chachu ya kuinua maisha ya washiriki wa mkutano huu." Mkutano huo umehudhuriwa na washiriki kutoka maeneo mbalimbali ya Wilaya ya Tarime huku Mgeni rasmi akiwa ni Mhe Mkuu wa Wilaya ya Tarime Meja Edward Gowele, ambapo wamepatiwa mafunzo juu ya mbinu bora za ...

Deo Meck Achangia Vifaa Katika Mkutano wa Wanawake na Vijana Wajasiriamali Tarime

Image
  Pichani ni mdau wa maendeleo Deo Meck Tarime, Mei 16, 2025 – Mdau wa maendeleo wa Wilaya ya Tarime, Deo Meck, ameonyesha moyo wa kujitoa kwa jamii kwa kuchangia vifaa muhimu kufanikisha mkutano wa wanawake na vijana wajasiriamali uliofanyika leo mjini Tarime. Katika mchango wake, Deo Meck ametoa dozen 18 za notebook na box 4 za kalamu, vifaa ambavyo vimetumika moja kwa moja katika mkutano huo ulioratibiwa na Tanzania Women Chamber of Commerce (TWCC). Mkutano huo umejikita katika kuwajengea uwezo wanawake na vijana wajasiriamali, kuwaunganisha na fursa za kiuchumi, mitaji na elimu ya ujasiriamali kwa ajili ya kukuza biashara zao. Akizungumza wakati wa hafla ya utoaji wa vifaa hivyo, Deo Meck alisema: "Ninaamini kuwa maendeleo ya jamii yanaanza kwa kuwawezesha wanawake na vijana. Mchango huu ni sehemu ya dhamira yangu ya kusaidia juhudi zao." Uongozi wa TWCC umeushukuru mchango huo na kumpongeza Deo Meck kwa kujitokeza kuwasaidia vijana na wanawake kwa vitendo. Mkutano huo um...

TAASISI YA MARAFIKI WA MAENDELEO TARIME YAMWAGA VIFAA VYA TAALUMA VYENYE THAMANI YA MILIONI 40 KWA SHULE MBILI TARIME VIJIJINI

Image
    Na Daniel Mussa – Tarime Kwa lengo la kuunga mkono juhudi za kuinua kiwango cha elimu katika Wilaya ya Tarime Vijijini, Taasisi ya Marafiki wa Maendeleo Tarime imekabidhi vifaa vya kisasa vya kufundishia na kujifunzia vyenye thamani ya jumla ya shilingi milioni 40 kwa shule mbili za sekondari — Magoto na Mbogi. Kila shule imenufaika na kompyuta za mezani (desktop) mbili, kompyuta mpakato (laptop) moja kwa matumizi ya Mkuu wa Shule, na mashine moja ya kupiga nakala (photocopy machine) aina ya Canon. Vifaa hivyo vimepokelewa kwa furaha kubwa na walimu, wanafunzi na jamii inayozunguka shule hizo. Akikabidhi vifaa hivyo kwa niaba ya taasisi, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Marafiki wa Maendeleo Tarime, Ndugu Martine Marwa, aliishukuru bodi ya taasisi hiyo pamoja na wadau mbalimbali waliotoa michango yao kwa moyo wa uzalendo. “Tunaishukuru bodi ya taasisi yetu kwa kuratibu na kufanikisha upatikanaji wa vifaa hivi kupitia michango ya wadau wetu. Tunaamini kwamba uwekezaji katika e...