WAZIRI CHANA AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA MRADI WA REGROW KIHESA KILOLO

 



Na Happiness Shayo - Iringa 


Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi, Dkt. Pindi Chana (Mb) amefanya ziara ya kushtukiza katika mradi wa ujenzi wa kituo cha utalii cha Bodi ya Utalii Tanzania (TTB) na kituo cha utafiti cha Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) inayotekelezwa chini ya mradi wa Kuboresha Usimamizi wa Maliasili na Kukuza Utalii Kusini mwa Tanzania (REGROW), Kihesa Kilolo Mkoani Iringa.



Mhe. Chana amejionea maendeleo ya mradi huo ambapo mradi wa ujenzi wa kituo cha utalii wenye thamani ya shilingi bilioni 21.4 umefikia asilimia 31 na kituo cha utafiti chenye thamani ya shilingi bilioni 1.55 kimefikia asilimia 80.


Ikumbukwe kuwa mnamo Septemba 7, 2024 Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii ilifanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa miradi hiyo na kuelekeza Wakandarasi kusimamia mikataba yao na kukamilisha miradi hiyo kwa wakati.



Mhe. Chana yuko Mkoani Iringa kwa ziara ya kikazi ya kukagua miradi mbalimbali iliyo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii.

Comments

Popular posts from this blog

GWAJIMA AACHE KUCHEZEA AMANI YA TAIFA, NA MHE. RAIS SAMIA AANGALIE JICHO LA CHINI YA KIVULI HIKI

MKURUGENZI WA SOYA ONE LIMITED AWASISITIZA WAUMINI WA EAGT RONSOTI TARIME MJINI KUILINDA AMANI; AFANIKISHA UPATIKANAJI WA MCHANGO WA MILIONI 12, ACHANGIA MILIONI 8 NA ASINDIKIZWA KWA MILIONI 5

SOYA ONE LIMITED YAENDELEA KUNG’ARA KATIKA UDHAMINI WA ELIMU NA JAMII TARIME