WANANCHI JIANDIKISHENI KWENYE DAFTARI LA MKAZI
Mbunge Wa Viti Maalum Mkoa wa Mara *Mhe Agnes Mathew Marwa* amewataka wananchi Wa Tarime Na Tanzania Kiujumla kujiandikisha katika Daftari la mkaazi. Uchaguzi wa Serikali za Mitaa ni mhimu, tujiandikishe kwenye Orodha ya Mpiga kura wa Serikali za Mitaa katika Daftari la mkaazi liloanza Tarehe 11 - 20/10/2024 na ili kuweza kushiriki Uchaguzi. Wananchi Wote twende kujiandikisha wingi ili CCM ipate wapiga wa kutosha kwani DKT SAMIA SULUHU HASSAN NI FURAHA YETU 2025
Naomba wananchi katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania kujitokeza kwa wingi kujiandikisha katika Daftari la Mkaazi ili kuweza kupiga kura 27 November 2024
Wananchi wote nchini uchaguzi wa Serikali za mitaa 2024 ni uchaguzi mhimu sana kwani katika ngazi za vijiji, vitongoji na mitaa ndiko mipango ya wananchi hupangwa, hivyo wananchi tujiandikishe wengi katika vituo vya karibu au maeneo karibu na Unako Fanyia Biashara zako ili kuweza kupata nafasi ya kushiriki kupiga kura na kuchagua viongozi
KAMA UNA HABARI NA UNATAKA TUICHAPISHE HAPA TUTAFTE KUPITIA GMAIL moonglobal255@gmail.com WhatsApp +255656114499


Comments
Post a Comment